Jinsi ya Kupika Pilau Ya Samaki Wa Tuna Na Mboga

Vipimo
Mchele  - 2 Mugs      
Mboga mchanganyiko za barafu (Frozen veg)  - Mug
Tuna (samaki/jodari) -  2 kopo
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi -2 vijiko vya supu
Garam masala - 1 kijiko cha supu
Nyanya - 2  
Kitungu maji -   1
Mdalasini nzima -  2 vijiti
Karafuu  - 6 chembe
Pilipili mbichi  - 1
Chumvi - kiasi
Viazi - 3
Maji - 2 ½ Mugs
Mafuta -  3 vijiko vya supu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
  1. Osha mchele na uroweke kwa muda wa dakika 20
  2. Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown).
  3. Mimina viazi, thomu na tangawizi,  bizari zote na kaanga.
  4. Tia nyanya uliyokatakata ikaange mpaka iwive.
  5. Tia tuna endelea kukaanga kidogo tu.
  6. Tia maji, yatakapochemka tia mchele.
  7.  Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa ½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari  kuliwa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.